Sunday, March 24, 2013
Watumishi wa umma watakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika utendaji kazi
Sunday, March 24, 2013 by Unknown
Na Frank John – Maelezo
Watumishi wa umma wametakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa taaluma zao hasa katika kitengo cha manunuzi ili sekta binafsi ziweze kujifunza kutoka kwao.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na Kamishna wa Idara ya Manunuzi ya Umma kutoka wizara ya Fedha Dk. Fredrick Mwakibinga katika kongamano la kujadili rasimu ya sera ya manunuzi lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa JB uliopo jijini Dar es Salaam.
Dk Mwakibinga pia aliwataka Maafisa ugavi, wananchi na wadau mbalimbali kutoa maoni yao juu ya rasimu ya Sera ya manunuzi ya Umma ili waweze kufanikisha zoezi la mchakato wa uundwaji wa sera hiyo.
Alisema kuwa kupatikana kwa sera nzuri na ya kisasa ya manunuzi ya umma ambayo ni muongozo wa Serikali katika sekta hiyo, kutaisaidia Serikali kutimiza nia na malengo ya kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.
“Tunayo mambo mengi ya kuangalia kama Serikali ili kuboresha sekta hii, ikiwa ni pamoja na kuangalia miundo ya Idara za ugavi, idadi ya watumishi na kuwajengea uwezo wagavi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi”, alisema Dk. Mwakibinga.
Continue reading →

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Watumishi wa umma watakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika utendaji kazi”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.