Thursday, May 9, 2013
HATIMAYE DAVID MOYES ATHIBITISHWA RASMI KUMRITHI FERGUSON KWA MKATABA WA MIAKA 6
Thursday, May 9, 2013 by Unknown
Hatimaye Manchester United imethibitisha DAVID MOYES ndio atakuwa kocha mpya wa kumrithi Sir Alex Ferguson kwa mkataba wa miaka 6.Alex Ferguson jana alitangaza kustaafu kuifundisha timu hiyo aliyodumu nayo kwa takribani miaka 27 na akiwa anamtaja mrithi wake wake Fergie alisema: "Wakati tunajadili mtu wa kunirithi wote tulikubaliana kuhusu David Moyes.
"David ni mtu makini mwenye miiko ya kazi. Nimekuwa nikipenda ufanyaji wa kazi yake kwa muda mrefu na niliwahi kumshawishi mwaka 1998 ajiunge nami kuwa msaidizi wangu hapa. Akiwa kijana mdogo na akiwa ndio anaanza maisha yake ya ukocha na tangu wakati huo amekuwa akifanya kazi nzuri na klabu ya Everton.
"Hakuna swali kwamba ana kila ubora ambao tulikuwa tunautegemea kwa meneja mpya wa klabu hii.”- alisema Ferguson.
Tags:
michezo

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 Responses to “HATIMAYE DAVID MOYES ATHIBITISHWA RASMI KUMRITHI FERGUSON KWA MKATABA WA MIAKA 6 ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.