Friday, May 10, 2013
KESI YA MADAWA YA KULEVYA MUME WA JACK PATRICK ARUDI URAIANI
Friday, May 10, 2013 by Unknown
Na Imelda Mtema
MUME wa mwanamitindo maarufu hapa Bongo, Jacqueline Patrick, Abdullatif Fundikira ‘Tiff”, aliyekuwa jela ya Gereza la Keko jijini Dar alikokuwa akishikiliwa kwa tuhuma za kufanya biashara ya madawa ya kulevya, amerudi uraiani baada ya kupata dhamana.
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Tiff aliachiwa kwa dhamana Ijumaa iliyopita katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kusota ‘lupango’ kwa takriban mwaka mmoja.
“Ni kweli sasa hivi Tiff yuko mtaani, ametoka kwa dhamana ila kuhusiana na suala la ndoa yake amesema haipo tena, anaangalia maisha yake,” kilidai chanzo.
Katika kupata ukweli wa habari hii, mwandishi wetu alimpigia simu Abdullatif lakini hakupokea ila Jack alipopatikana alikiri zilipendwa wake huyo kuachiwa kwa dhamana.
credit- globalpublishers
Tags:
udaku

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KESI YA MADAWA YA KULEVYA MUME WA JACK PATRICK ARUDI URAIANI”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.