Sunday, June 16, 2013

Tazama Picha Za Washindi Wa Tuzo Za Washindi Wa Bongo Movies, Jb, Irene Uwoya, Ray Wang'ara Tuzo Za Bongo Moviez 2013


Mkurugenzi
wa Kampuni ya Steps, Diresh Solanki akimpa tuzo msanii bora wa kiume 
katika tasnia ya filamu nchini Jacob Steven JB wakati wa utoaji wa tuzo 
hizo zilizofanyika usiku wa kuamkia leo na kuhudhuliwa na wasanii wengi 
nchini hii ni kwa mara ya kwanza steps inaandaa tuzo hizi zitakazokuwa 
zikitolewa kila mwaka.Picha nawww.burudan.blogspot.com

Pazia ra Tuzo za Steps Bongo Movie Awards ukiwa umefunguliwa na waziri wa Sayansi na Teknolojia Makame Mbawala 




Mzee Majuto akipokea Tuzo ya msanii bora wa uchekeshaji 

Msanii Steve Nyerere akipokea Tuzo 

Msanii Nice Mohamedi 'Mtunis' akipokea tuzo ya Mwaka 2012 zilizoandaliwa kwa mara ya kwanza na kampuni ya Steps Entatainment tuzo hizi zitakazokuwa zikitolewa kila mwaka.Picha na www.burudan.blogspot.com
MAMA SHILOLE AKIWA JUKWAANI 


Mtoto Jenifa akichukua tuzo yake 

Riyama akipokea tuzo yake 
Msanii Niva akichukua TUZO ya msanii bora Chipkizi kulia yupo msanii mwenzake Rado 

Mjumbe
wa Kamati ya saidia Taifa Stars Ishinde, Ridhiwani Kikwete kushoto 
akimkabidhi tuzo Haji Adamu kwa niaba ya Jimmy Mponda aliyeshinda msanii
bora wa Filamu za Mapigano wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika 
kwa mara ya kwanza nchini na kuandalia na kampuni ya Steps Picha na www.burudan.blogspot.com

Mjumbe
wa Kamati ya saidia Taifa Stars Ishinde, Ridhiwani Kikwete wa tatu 
kushoto akiwapongeza baadhi ya wasanii wa marehemu Kanumba baada ya 
kuwakabizi tuzo

Mkurugenzi
wa Kampuni ya Steps Dilesh Solanki akimkabizi tuzo ya mwongozaji bora 
wa filamu nchini kwa mwaka 2012 Vicent Kigosi 'Ray ' wakati wa utoaji wa tuzo hizo zilizofanyika usiku wa kuamkia jana usiku.

Mkurugenzi
wa Kampuni ya Steps Dilesh Solanki akifafanua jambo baada ya kumkabizi 
tuzo Vicent Kigos 'Ray' ya mwogozaji bora wa filamu nchini kwa mwaka 
2012. 


Wafanyakazi wa Kampuni ya Steps wakipokea tuzo 

Baadhi
ya wasanii wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa tuzo zao 
za kwanza kwa mwaka 2012 zilizozaminiwa na kampuni ya steps. 

MPIGA PICHA MOHAMED ARALAKIA ZA COVERS MBALIMBALI ZA KAMPUNI YA STEPS AKIPOKEA TUZO 

:KAMPUNI ya 
Usambazaji wa filamu ya Steps Entatainment ya jijini Dar es salaam 
mwishoni mwa wiki iliyopita ilitoa tuzo kwa wasanii bora waliofanya 
vizuri katika tasnia ya filamu nchini kwa mwaka 2012 ikiwa ni kwa mara 
ya kwanza kuanzishwa kwa tuzo hizo

Akizungumzia tuzo hizo 
Mkurugenzi wa Kampunu hiyo Direshi Solanki amesema kuwa tuzo hizo 
watakuwa wakizitoa kila mwaka kwa kuleta maendeleo ya filamu nchini 
kampuni hiyo iliyojikita katika kusambaza filamu za wasanii wameweka 
historia ya kuigwa kutokana na kuanzisha tuzo hizo

Baadhi ya 
washindi ambao waliopatikana katika tuzo hizo wa kwanza ni 
Steven Mangendela 'Steve Nyerere', Issa Mussa 'Cloud 112' Mohamed 
Nurdini 'Chek budi' Nice Mohamed 'Mtunisi' Irene Paul akinyakuwa msanii 
bora chipukizi wa kike

Wakati katika kinyanganyiro cha kumpata 
msanii bora wa kiume alinyakuwa Jacob Stevin 'JB' huku msanii bora wa 
kike ikienda kwa mwana dada Irene Uwoya, na msanii bora wa filamu za 
mapingano ilikwenda moja kwa moja kwa Jimmy Mponda 'Jimmy Masta'

Wakati katika kipengere cha muhongozaji bora wa filamu kilikwenda kwa vicent Kigosi' Ray' na kampuni yake ya RJ Filamu

Mbali
na hivyo kulikuwa na tuzo za heshima kwa wasanii waliofanya vizuri 
lakini kwa sasa hawapo duniani moja ni kwa Stevin Kanumba,Saidi Kilowoko
'Sajuki' John Stefano, Hussein Ramadhani Mkiety 'Sharo Milionea'

Katika utoaji wa tuzo huzo kulikua na burudani nyingi zikiongozwa na Odama Bendi

Tags:

0 Responses to “ Tazama Picha Za Washindi Wa Tuzo Za Washindi Wa Bongo Movies, Jb, Irene Uwoya, Ray Wang'ara Tuzo Za Bongo Moviez 2013”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI