Wednesday, August 7, 2013

VIDEO:MWANAUME APOTELEWA NA NYETI, YARUDI NDOGO NA ISIYOKUWA NA NGUVU


MWANAUME mmoja aliyejulikana kwa jina la Elias Peter (28) mkazi wa Mwananyamala Msisiri, Dar hivi karibuni alijikuta katika wakati mgumu baada ya uume wake kutoweka kwa siku tatu na kurudi ambao hauna nguvu.
Akizungumza na paparazi wetu, Elias alisema siku ya tukio alipewa sigara na kijana mmoja anayejulikana kwa jina la Saleh Mtima alipomaliza kuvuta alianza kuhisi baridi kali ghafla akajishtukia uume haupo amebaki ‘flat’.
Baada ya hapo alikaa siku tatu bila uume kurudi ndipo akaamua kwenda kumueleza na kumuomba ushauri mzee mmoja anayeheshimika sana eneo hilo anayejulikana kwa jina la Mfinanga Kishegwe  akamweleza kuwa  kilichompata ni mashetani ila uume utarudi.
“Baada ya kusubiri kwa siku tatu nilienda kuomba ushauri kwa mzee Mfinanga ambaye aliniambia utarudi na baada ya muda kweli ulirudi lakini ulikuwa mdogo kama wa mtoto na haukuwa na nguvu jambo ambalo limepelekea pale mtaani ninapoishi kila nikipita watu wananizomea na kuniita mwanamke,”alisema Elias.
(Habari/Picha/Video : Na Gladness Mallya / GPL)

ANGALIA VIDEO HAPA:

Tags:

0 Responses to “VIDEO:MWANAUME APOTELEWA NA NYETI, YARUDI NDOGO NA ISIYOKUWA NA NGUVU”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI