Friday, February 21, 2014
ALICHOSEMA BERNARD MEMBE JUU YA MGOGORO WA MPAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI
Friday, February 21, 2014 by Unknown
Tanzania bado ipo kwenye mgogoro na nchi ya Malawi juu ya mpaka halisi wa nchi,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Benard Membe amesema hatma juu ya mgogoro huo inategemewa kutolewa mwezi march.
Hukumu hiyo itaamuliwa baada yajopo la Usuluhishi litakapokaa na kusikiliza pande zote mbili ambalo litaongozwa na Rais wa zamani wa Msumbiji Joachim Chisano
Kupatikana kwa suluhu ya mgogoro wa mpaka huo kutawatoa hofu wananchi wanaoishi pembezoni mwa Ziwa hilo ambao wamekuwa wakitegemea shughuli za uvuvi wakiwemo wakazi wa kijiji cha Manda Jimbo la Ludewa mkoani Njombe.
Wakazi wa eneo hilo wamesema kwa hivi karibuni tangu kutulia kwa vuguvugu la mgogoro huo wamekuwa wakiendelea shughuli zao za maendeleo kama kawaida ikiwemo uvuvi.
Tags:

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 Responses to “ALICHOSEMA BERNARD MEMBE JUU YA MGOGORO WA MPAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.