Friday, February 21, 2014

ALICHOSEMA BERNARD MEMBE JUU YA MGOGORO WA MPAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI



Tanzania bado ipo kwenye mgogoro na nchi ya Malawi juu ya mpaka halisi wa nchi,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Benard Membe amesema hatma juu ya mgogoro huo inategemewa kutolewa mwezi march.
Hukumu hiyo itaamuliwa baada yajopo la Usuluhishi litakapokaa na kusikiliza pande zote mbili ambalo litaongozwa na Rais wa zamani wa Msumbiji Joachim Chisano
Kupatikana kwa suluhu ya mgogoro wa mpaka huo kutawatoa hofu wananchi wanaoishi pembezoni mwa Ziwa hilo ambao wamekuwa wakitegemea shughuli za uvuvi wakiwemo wakazi wa kijiji cha Manda Jimbo la Ludewa mkoani Njombe.
Wakazi wa eneo hilo wamesema kwa hivi karibuni tangu kutulia kwa vuguvugu la mgogoro huo wamekuwa wakiendelea shughuli zao za maendeleo kama kawaida ikiwemo uvuvi.

Tags:

0 Responses to “ALICHOSEMA BERNARD MEMBE JUU YA MGOGORO WA MPAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI