Saturday, March 23, 2013

Jiungeni na NHIF/CHF kulinda mitaji yenu-Mkurugenzi



Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Adolph Mapunda akifungua mafunzo ya akina mama wajasiriamali wilayani Kilwa yaliyoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF). Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Raphael Mwamoto akitoa maelezo ya utangulizi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu. Mkurugenzi wa kitengo cha Uwezeshaji Wanawake katika Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Tabu Likoko akieleza jambo kwa washiriki wa mafunzo. Mmoja wa washiriki akiuliza swali Mmoja wa washiriki akiuliza swali

………………………………………………………………………

Na Mwandishi Wetu

WANAWAKE wilayani Kilwa hususan wajasiriamali, wametakiwa kuchangamkia fursa ya kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii ili kulinda mitaji yao wakati wanapougua.

Wametakiwa kufanya hivyo kutokana na ukweli kwamba, watanzania wengi hawana utamaduni wa kujiwekea akiba hasa ya matibabu hali inayolazimu kutumia fedha za biashara wakati wanapopatwa na matatizo ya ugonjwa.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilwa, Adolph Mapunda wakati akifungua mafunzo ya akina mama wajasiriamali wilayani humo yaliyoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya yanayowaelimisha umuhimu wa kuwa kwenye mfumo wa kupata huduma za matibabu kupitia bima za afya.

Mapunda alisema kuwa kwa sasa gharama za matibabu zimekuwa zikipanda kila kukicha hivyo njia pekee inayoweza kuwakomboa ni kuwa kwenye utaratibu wa NHIF au CHF utaratibu ambao ni wa kuchangia kabla ya kuugua.

Hata hivyo alisema kuwa uongozi wilayani humo utaendelea na jitihada za uelimishaji wananchi ili waweze kutumia fursa hii ambayo ni njia pekee ya kuwakomboa kwenye suala zima la afya.

“Kundi lenu ni muhimu sana siyo tu katika kuinua hali ya uchumi wa nchi hii, bali pia katika kuziwezesha familia zenu katika suala zima la afya, mkijiunga na huduma hizi mtakomboa familia zenu na mtaweza kupanga hata mipango ya familia huku mkiwa na uhakika wa matibabu pale ugonjwa unapotokea,” alisema Mapunda.

”Naamini kuwa wengi wenu hapa mumewahi kupatwa na shida ya kuugua au kuuguliwa wakati mkiwa hamna kitu mfukoni na hivyo kulazimika kuuza vitu vya ndani au kuua mtaji wa biashara ili kumuhudumia mgonjwa hivyo tumieni fursa hii,” alisema.

Continue reading →

Tags:

0 Responses to “Jiungeni na NHIF/CHF kulinda mitaji yenu-Mkurugenzi ”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI