Saturday, March 23, 2013
Jiungeni na NHIF/CHF kulinda mitaji yenu-Mkurugenzi
Saturday, March 23, 2013 by Unknown
………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
WANAWAKE wilayani Kilwa hususan wajasiriamali, wametakiwa kuchangamkia fursa ya kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii ili kulinda mitaji yao wakati wanapougua.
Wametakiwa kufanya hivyo kutokana na ukweli kwamba, watanzania wengi hawana utamaduni wa kujiwekea akiba hasa ya matibabu hali inayolazimu kutumia fedha za biashara wakati wanapopatwa na matatizo ya ugonjwa.
Rai hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilwa, Adolph Mapunda wakati akifungua mafunzo ya akina mama wajasiriamali wilayani humo yaliyoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya yanayowaelimisha umuhimu wa kuwa kwenye mfumo wa kupata huduma za matibabu kupitia bima za afya.
Mapunda alisema kuwa kwa sasa gharama za matibabu zimekuwa zikipanda kila kukicha hivyo njia pekee inayoweza kuwakomboa ni kuwa kwenye utaratibu wa NHIF au CHF utaratibu ambao ni wa kuchangia kabla ya kuugua.
Hata hivyo alisema kuwa uongozi wilayani humo utaendelea na jitihada za uelimishaji wananchi ili waweze kutumia fursa hii ambayo ni njia pekee ya kuwakomboa kwenye suala zima la afya.
“Kundi lenu ni muhimu sana siyo tu katika kuinua hali ya uchumi wa nchi hii, bali pia katika kuziwezesha familia zenu katika suala zima la afya, mkijiunga na huduma hizi mtakomboa familia zenu na mtaweza kupanga hata mipango ya familia huku mkiwa na uhakika wa matibabu pale ugonjwa unapotokea,” alisema Mapunda.
”Naamini kuwa wengi wenu hapa mumewahi kupatwa na shida ya kuugua au kuuguliwa wakati mkiwa hamna kitu mfukoni na hivyo kulazimika kuuza vitu vya ndani au kuua mtaji wa biashara ili kumuhudumia mgonjwa hivyo tumieni fursa hii,” alisema.
Continue reading →

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Jiungeni na NHIF/CHF kulinda mitaji yenu-Mkurugenzi ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.