Sunday, March 24, 2013

ULIMWENGU, SAMATTA WANG’ARA STARS IKIITUNGUA MOROCCO TATU




Timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika mechi ya awali kuwania kucheza Kombe la Dunia.


Stars imefanikiwa kuibuka na ushindi huo mnono baada ya kuwachapa Morocco katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja Taifa jijini Dar es Salaam.


Mabao ya Stars yamefungwa na Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta, wote wawili ni washambuliaji wa TP Mazembe ya DR Congo.


Pamoja na kuifunga Morocco, kikosi cha Stars chini ya Kocha Kim Poulsen kilitawala mchezo kwa muda mwingi na mashabiki walionyesha uzalendo kwa kuwashangilia mwanzo mwisho.


Stars iko katika kundi moja na Ivory Coast, Gambia na Morocco na ushindi huo umewafanya wakae kileleni mwa kundi hilo.

CREDIT- SALEH JEMBE

Tags:

0 Responses to “ULIMWENGU, SAMATTA WANG’ARA STARS IKIITUNGUA MOROCCO TATU”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI