Sunday, May 5, 2013
UVCCM Arusha wazidi kushambuliana.
Sunday, May 5, 2013 by Unknown
Arusha.
Sakata la Kaimu Katibu wa UVCCM Arusha, Masoud Rajabu kukamatwa na kisha kupewa kipigo na viongozi wenzake ndani ya umoja huo, limechukua sura mpya baada viongozi wa umoja huo kushambuliana vikali kwa kutoleana lugha za matusi
Masoud alishambuliwa kwa kupigwa na viongozi wenzake hivi karibuni mara baada ya kutuhumiwa kukusanya fedha za miradi mbalimbali bila idhini ya uongozi wa jumuiya hiyo, ambapo mbali na kupigwa pia aliporwa kiasi cha Sh140,000 na viongozi hao.
Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gazeti hili, mara baada ya tukio hilo Mwenyekiti wa UVCCM Arusha, Robinson Meitinyiku aliamua kuitisha kikao cha pamoja juzi kujadili tukio hilo.
Habari zilidai kuwa mara baada ya wajumbe kuwasili kikaoni, ndipo mwenyekiti wa umoja huo mkoani hapa aliwasomea ajenda za kikao lakini wakati wa kuchangia ndipo hali ya hewa ilianza kuchafuka.
Tags:
siasa

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 Responses to “UVCCM Arusha wazidi kushambuliana. ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.