Home
» michezo
» Fabregas Azikata Maini Arsenal Na Man United: Siondoki Barcelona Ng’oo Labda Walazimishe Kuniuza
Tuesday, June 11, 2013
Fabregas Azikata Maini Arsenal Na Man United: Siondoki Barcelona Ng’oo Labda Walazimishe Kuniuza
Tuesday, June 11, 2013 by Unknown
CESC FABREGAS amesisitiza kuwa ataondoka Barcelona iwapo tu watamchoka na kulazimisha kumuuza.
Fabregas ambaye alijunga na Barcelona kwa pauni milioni 40 kutoka Arsenal mwaka 2011, amekuwa akihusishwa kurejea Ligi kuu ya Uingereza, huku kipaumbele kikiwekwa zaidi kwa Arsenal ingawa Manchester United nao wamo.
Lakini Fabregas amesema: “Imenichukua muda mrefu kufika hapa nilipo, na sitegemei kuitupa nafasi hii kirahisi.
“Kama Barcelona watasema hawanihitaji hilo litakuwa ni jambo lingine – lakini shida yangu ni kubakia Barca.
“Imekuwa ni njozi yangu tangu utotoni. Barcelona ni nyumbani kwangu na siku zote nimekuwa nikiota kushinda mataji hapa.”
Fabregas alikosolewa na mashabiki wa Barcelona katika msimu wake wa kwanza kurejea nyumbani.
Alisema: “Baadhi ya watu wanaweza wakawa hawavutiwi na uchezaji wangu lakini linanipa changomoto ya kujituma zaidi.
“Kama mashabiki wananizomea, nahitaji kulipokea hilo. Nilikuwa mtu wa kwanza kujua kuwa hii itakuwa changamoto kubwa katika maisha yangu. Nataka kucheza.”

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 Responses to “Fabregas Azikata Maini Arsenal Na Man United: Siondoki Barcelona Ng’oo Labda Walazimishe Kuniuza”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.