Monday, June 10, 2013
TCRA YAAGIZA STAR TV IRUDISHWE MARA MOJA KATIKA VING'AMUZI VYA STAR TIMES
Monday, June 10, 2013 by Unknown
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Prof. John Nkoma akitoa maamuzi kuhusu kujitoa kwa Star TV kwenye Star Times.
TCRA imeagiza Chaneli ya Star Tv irudishwe mara moja kwenye Star Times ndani ya masaaa machache yajayo.
Aidha Star Times na Star TV wameelezwa kuwa wote wamevunja sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya 2010 na Kanuni zake na kutakuwa na kujitetea tarehe 17 Juni 2013.
Agizo la kurudishwa kwa Chaneli ya Star TV linatakiwa kutekelezwa ili kuhakikisha kuwa wananchi hawanyimwi haki ya kupata habari.
Vile vile wote wametakiwa kufuata Sheria inapotokea kutokuafikiana badala ya kutoa maamuzi bila kumshirikisha Mdhibiti (TCRA)
Tags:
kitaifa

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

0 Responses to “TCRA YAAGIZA STAR TV IRUDISHWE MARA MOJA KATIKA VING'AMUZI VYA STAR TIMES ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.