Friday, July 19, 2013

MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTRE AMWAGIWA TINDIKALI





HABARI ZIMETUFIKIA PUNDE TU ZINASEMA MFANYABIASHARA MMOJA MAARUFU NCHINI AMEMWAGIWA KITU KINACHODHANIWA NI TINDIKALI NA WATU WASIOJULIKANA MAENEO YA MSASANI JIRANI NA KITUO CHA POLISI CHA OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM.


JINA LA MFANYABIASHARA HUYO BADO HALIJAJULIKANA, NA HATA POLISI BADO HAWAJAKANUSHA WALA KUTHIBITISHA TUKIO HILO LINALOSEMEKANA LILILOTOKEA BAADA YA MUDA WA KUFUTURU KUMALIZIKA.




AIDHA, WANAHABARI WETU WAMESHUHUDIA MAGARI KADHAA YA POLISI YAKIWA KWENYE MAEGESHO YA DUKA MOJA KUBWA LILILOPO MAENEO KARIBU NA OYSTERBAY POLICE, AMBAKO HAKUNA ALIYETAKA KUSEMA CHOCHOTE, JAPO HABARI ZINASEMA HAPO NDIPO TUKIO LILIPOTOKEA.




JUHUDI ZA KUMSAKA KAMANDA WA POLISI MKOA WA KINONDONI AMA KAMANDA WA KANDA MAALUMU YA DAR ES SALAAM AFANDE SULEIMAN KOVA ZINAENDELEA. NASI TUTAWAJULISHA KILA TUTAPOPATA HABARI ZAIDI.

Taarifa za awali zinadai kwamba Mfanyabiashara Said Mohamed Saad ambaye ni Mmiliki wa Home Shopping Centre (Dar), amwagiwa tindikali saa mbili ya usiku huu maeneo ya Msasani City Mall ....

Taarifa hizo zinadai kwamba mtuhumiwa aliyefanya kitendo hicho alitoka mbio, mlinzi akamkimbiza lakini bahati mbaya akateleza na kuanguka na jamaa akawahi pikipiki na kutoweka eneo la tukio,


Source: Michuzi Blog

Tags:

0 Responses to “MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTRE AMWAGIWA TINDIKALI ”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI