Thursday, April 4, 2013
WEMA SEPETU AZIDI "KUMPROMOTE" KAJALA MASANJA
Thursday, April 4, 2013 by Unknown
Muigizaji na Miss Tanzania wa zamani Wema Sepetu amesema licha ya kumsainisha Kajala Masanja kwenye kampuni yake, hategemei kumfanyisha kazi kurudisha shilingi milioni 13 alizomtolea kwenye hukumu yake.
Akiongea kwenye kipindi cha XXL, Wema amesema Kajala atakuwa akifanya kazi zake lakini atakuwa akimlipa kama kawaida. Kwa kuanza Kajala ataigiza kama mhusika mkuu kwenye filamu iitwayo Princess Sasha.
“Tutaenda kuishoot nje ya Dar, ninataka kuishoot mandhari fulani hivi kama ya kijijini. Ni mtoto wa mfalme, Kajala ndo atakuwa Princess Sasha, she is going to be the main character, “ alisema Wema.
Kwa upande wake Kajala amesema aliamua kujichora tattoo ya jina la Wema kwasababu anamchukulia kama shujaa.
“Mi naweza kusema nimeichora kuonesha nimeappreciate vipi kitu alichonifanyia , watu wengine wanaichukulia vibaya, wataongea vibaya, lakini mimi najua moyoni mwangu. Sababu nimeona siwezi kumlipa hiyo hela sasa hivi.
Ntamkumbuka siku zote hata chochote kikitokea atabakia kuwa mtu… yaani she is my hero.”
Tags:
burudani ,
udaku
This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WEMA SEPETU AZIDI "KUMPROMOTE" KAJALA MASANJA ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.