Tuesday, May 7, 2013

JAJI MSTAAFU EUSEBIA NICHOLAUS MUNUO ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BODI YA TAIFA YA PAROLE




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Simu: +255-22-2112035/40 S.L.P. 9223
Nukushi: +255-2122617/2120486 Dar es Salaam
Barua pepe: ps@moha.go.tz
06 Mei 2013


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya Kifungu cha 3(2) (a) cha Sheria ya Bodi ya Parole Sura 400 amemteua Jaji Mstaafu Eusebia Nicholaus Munuo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole kuanzia tarehe 24 Aprili, 2013. Mheshimiwa Eusebia Nicholaus Munuo ni Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania.

Sambamba na uteuzi huo Mhe. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya kifungu 3(2)(f) cha Sheria hiyo, amewateua Bw.John William Nyoka na Bw. Fransis Stolla kuwa wajumbe wa Bodi hiyo. Bw. John William Nyoka ni Naibu Kamishna wa Magereza Mstaafu na kabla ya kustaafu kwake alikuwa Mshauri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, nchini Namibia kama Mshauri wa Magereza na Bw. Fransis Stolla ambaye ni Wakili wa Kujitegemea na kwa sasa ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika(Tanganyika Law Society).

Wajumbe hawa pamoja na Mkurugenzi wa Mashtaka, Mkemia Mkuu wa Serikali, Kamishna wa Ustawi wa Jamii na Mjumbe mmoja kutoka Ofisi ya Rais ndio wanaounda Bodi ya Taifa ya Parole kwa mujibu wa kifungu cha 3(2) cha Sheria hiyo.

Mbarak Abdulwakil 

Katibu Mkuu

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Tags:

0 Responses to “JAJI MSTAAFU EUSEBIA NICHOLAUS MUNUO ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BODI YA TAIFA YA PAROLE”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI