Sunday, May 12, 2013
Watangazaji/Maripota Hawa Walipataje Kazi?
Sunday, May 12, 2013 by Unknown
Ni muda mrefu sasa kumekuwa na wimbi la watangazaji au maripota wa television na radio wasiomudu kutamka maneno ya kiswahili wanapokuwa wakiripoti/wakitangaza au wakisoma hasa taarifa ya habari.Hii imekuwa kero unapomsikia ripota anatamka maneno mfano bizaa(bidhaa),feza(fedha)saman i(thamani)taalifa(taarifa)n.k. Kifupi matumizi ya r/l,th/s na dh/z ni kero iliyopitiliza kwa hawa watu kwani huondoa ladha ya matamshi ya kiswahili.Sasa swali ninalojiuliza ni vp watu hawa walifaulu usaili(interview)ktk vituo husika na zaidi wanaendelea kuharibu tu.Walifaulu vp mitihani yao tangu shule za msingi mpaka kupata kufikia elimu ya juu? Je maboss hawawasikizi wakawarekebisha? on job trainning hakuna?hata daily briefing pia hakuna?Enyi waandishi nguli mlioko humu jamvini tusaidieni kujadili.
Tags:
kitaifa

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Watangazaji/Maripota Hawa Walipataje Kazi? ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.