Thursday, June 27, 2013
Chadema wamjibu Waziri Mkuu
Thursday, June 27, 2013 by Unknown

Waziri Mkuu,Mizengo Pinda
Dodoma. Chama cha Maendeleo, Chadema kimeibuka jana bungeni na kusema Serikali inafahamu ukweli wa mlipuko wa bomu uliotokea katika mkutano wa chama hicho jijini Arusha.
Chama hicho kimesema Serikali ilitumia kutokuwepo kwao bungeni kupotosha wananchi kuhusu hali halisi juu ya mlipuko wa bomu hilo uliotokea wakati chama hicho kikihitimisha kampeni zake za uchaguzi mdogo wa udiwani katika Viwanja vya Soweto jijini Arusha, Juni 15, mwaka huu.
Akizungumza kabla ya kuanza kuchangia muswada wa sheria ya fedha ya mwaka 2013/2014, Waziri kivuli wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi wa Chadema, Halima Mdee alisema, “Kabla sijaanza kuchangia Mheshimiwa Spika naomba nianze kwa kuwapa pole wakazi wote wa Arusha kutokana na mlipuko wa bomu uliosababisha watu kupoteza maisha, kwani tangu limetokea tukio hilo leo ndiyo nazungumza kwa mara ya kwanza,”
“Tunazilaani kauli potofu zilizotolewa na Serikali hapa bungeni, Serikali inajua nini kilichotokea Arusha na ilitumia kutokuwepo kwetu kupotosha,” alisema.
CREDIT-MWANANCHI.COM
Tags:
kitaifa ,
siasa
CREDIT-MWANANCHI.COM

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “Chadema wamjibu Waziri Mkuu ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.