Monday, September 30, 2013
MAJAMBAZI WAVAMIA BENK JIJINI DAR ES SALAAM NA KUPORA ZAIDI YA MILIONI 150
Monday, September 30, 2013 by Unknown
Majambazi saba akiwemo mmoja ambaye amevalia sare za polisi wameiteka benki ya I&M jijini Dar es Salaam na kuchukuwa fedha zinazohisiwa kuwa ni zaidi ya shilingi milioni 150 na kutokemea kusikojulikana.
Tukio hilo limetokea katika benki hiyo iliyoopo katika makutano ya mtaa wa Indira Gandi na Mosque ambapo baadhi ya mashuhuda wameelezea tukio hilo lilivyokuwa.
Akizungumza katika eneo la tukio kamanda wa polisi mkoa wa Ilala kamanda Marieta Minagi amesema bado wanaendelea kufanya uchunguzi wa tukio lenyewe ingawa mpaka sasa ni kama milioni zaidi 150 zinahisiwa kuibiwa.
Naye mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meki Sadiki akiwa katika eneo hilo amesema matukio ya Kuiba fedha katika benki yanazidi kushamiri na hivyo kuna haja ya taasisi husika kujipanga upya.
Hata hivyo ITV ilishuhudia baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakipandishwa katika gari la polisi lenye namba za usajili T220 AMV na kuondoka nao kwa ajili ya mahojiano zaidi.
Tags:
kitaifa

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAJAMBAZI WAVAMIA BENK JIJINI DAR ES SALAAM NA KUPORA ZAIDI YA MILIONI 150”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.