Monday, June 17, 2013
DIWANI ARUSHA ASIMULIA ALIVYOLIPULIWA NA BOMU
Monday, June 17, 2013 by Unknown

Bille ambaye kwa sasa anaishi akiwa na vipande vya chuma mwilini alisema kuwa,kabla ya mfuko huo kutua ardhini alifikiri ni jiwe kwa kuwa alikuwa mita tatu tu kutoka ulipotua lakini ghafla alishangaa kuona ukilipuka na kumjeruhi vibaya.
“Wakati nikiwa pale jukwaani niliona mfuko mweusi ukipepea angani nikahisi ni jiwe limerushwa ghafla ulitua karibu na nilipokuwa lakini nikasikia mlipuko ghafla na kuna vyuma vikanirukia ,”alisimulia Bille.
Hata hivyo,alisema kuwa hakumwona mtu aliyerusha mfuko huo lakini ulitokea upande wa Baa ya Soweto iliyokuwa mkabala na jukwaa kuu upande wa Magharibi.
Akiendelea kusimulia alisema kwamba mara baada ya mfuko huo kulipuka alipigwa na vipande vya chuma katika eneo la kifua chake na mkono wa kulia na kisha kupoteza fahamu na kujikuta akiwa hospitali ya Selian.
Hata hivyo,alisema kuwa anakumbuka wakati akiwa jukwaani kulikuwa na amani ya kutosha na neno la mwisho analolikumbuka lilitamkwa na Mwenyekiti wa Chadema,Freeman Mbowe ambapo aliwataka watu wakichangie chama chao fedha za kuwawezesha kumaliza uchaguzi salama.
“Pale jukwaani nakumbuka kulikuwa na amani kabisa lakini nakumbuka neno la mwisho alilosema mwenyekiti wangu kwamba watu wachangie fedha za kukisaidia chama kishinde uchaguzi,”alisisitiza Bille
Diwani huyo kwa unyonge alisema kuwa baaya kufikishwa hospitalini hapo madaktari walimwambia ya kwamba ameonekana na vipande vya chuma mwilini ambavyo vimeingia umbali wa inchi mbili na wanasubiria visogee ili viweze kutolewa.
TOA MAONI YAKO HAPA
Tags:
kitaifa ,
siasa

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “DIWANI ARUSHA ASIMULIA ALIVYOLIPULIWA NA BOMU ”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.