Friday, July 12, 2013

"NAOLEWA KWA AJILI YA STAREHE ZA MAPENZI NA SI KWA AJILI YA KUZAA"...NATASHA WA BONGO MOVIE



MWIGIZAJI mkongwe wa maigizo na filamu Bongo, Suzan Lewis ‘Natasha’ ambaye pia ni mtangazaji wa Radio Times FM, anayetarajia kufunga ndoa kesho, amefunguka kuwa anaoelewa kwa ajili ya kustarehe na siyo kwenda kuzaa kama wengine wanavyofanya.

Akizungumza na mwandishi wetu, Natasha alisema kuwa katika maisha yake hakuna kitu anachokichukia kama kubeba mimba na umri alionao ndiyo kabisa hawezi kufanya hivyo bali atalea wajukuu tu.

“Kuolewa si lazima kuzaa, mimi nimeolewa kwa ajili ya ‘ku-relax’ na kufurahi maisha kwa mume wangu na si vinginevyo, wakati wa kuzaa umeshapita, namwachia Monalisa (mwanaye) sasa aendelee kuijaza dunia,” alisema Natasha.

Mwanamama huyo ambaye hivi karibuni alifanyiwa bonge la pati katika sherehe ya kuagwa ‘send-off’ katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar alisema kuwa anaiombea ndoa yake idumu miaka mingi, wafe wazikane.

Tags:

0 Responses to “"NAOLEWA KWA AJILI YA STAREHE ZA MAPENZI NA SI KWA AJILI YA KUZAA"...NATASHA WA BONGO MOVIE ”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI