Friday, August 30, 2013
ETOO NI MALI YA CHELSEA..NANI ANABISHA?
Friday, August 30, 2013 by Unknown

Eto’o aliingia London usiku wa kuamkia leo kwa usafiri wa treni toka nchini Urusi alikokuwa anaichezea klabu ya Anzhi Makhachkhala ambayo imemruhusu kujiunga na Chelsea kwa usajili wa bure.
Usajili huo unakuja siku moja baada ya The Blues kuthibitisha kukamilika kwa usajili wa kiungo mshambuliaji Willian ambaye amesajiliwa kwa paundi milioni 30 .
Eto’o anatarajiwa kusaini mkataba wa mwaka moja ndani ya Chelsea ambapo atalipwa paundi milioni 7 kwa mwaka baada ya kufikia makubaliano ya punguzo la mshahara toka paundi milioni 17 kwa mwaka alizokuwa analipwa nchini Urusi ambazo zilimfanya kuwa mchezaji anayelipwa fedha nyingi kuliko wote duniani .
Usajili wa Eto’o unakuja kama mpango mbadala wa Mourinho kusajili mshambuliaji ambaye amekuwa akimtaka baada ya kuthibitisha kumkosa Wayne Rooney wa Manchester United ambaye ameamua kubakia kwenye klabu yake .
Eto’o anaungana na Mourinho kwa mara ya pili baada ya kuchezea kwa mafanikio makubwa wakati wakiwa na Inter Milan ambapo klabu hiyo ya Italia ilitwaa mataji matatu katika msimu wa mwaka 2009/2010 .
Tags:
michezo

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ETOO NI MALI YA CHELSEA..NANI ANABISHA?”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.