Home
» kimataifa
» MWANAMKE ALIYEFANANISHWA NA KINARA WA MAUAJI YA WESTGATE AJITOKEZA NA KUKANUSHA HABARI HIYO
Wednesday, September 25, 2013
MWANAMKE ALIYEFANANISHWA NA KINARA WA MAUAJI YA WESTGATE AJITOKEZA NA KUKANUSHA HABARI HIYO
Wednesday, September 25, 2013 by Unknown
Kufuatia mashambulizi ya kigaidi katika mall ya West Gate jijini Nairobi, kumekuwepo na uvumi kuhusu mwanamke wa Uingereza aitwaye Samantha Lewthwaite au ‘White Widow’ kuhusika na tukio hilo. Jana kulikuwa kumekuwa na picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii pamoja na kuripotiwa na baadhi ya vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mtandao wa Mail Online wa Uingereza, za mwanamke ambaye baadhi ya watu waliamini kuwa ni Samantha Lewthwaite au ‘White Widow’.
Habari iliyokuwa inasambaa ni kuwa mwanamke huyo aliyedhaniwa kuwa ‘white widow’ alitoroka kwa njia ya kujifanya kumsaidia mwanamke huyo (kwenye picha hapo juu).
NTV ya Kenya iliamua kusahihisha habari hiyo kwa kumtafuta mwanamke huyo (kushoto katika picha) na walifanikiwa kumpata na kuweka taarifa hiyo sawa kwa kukanusha kutokuwa mtu ambaye watu walimdhania.
Akiongea na NTV Mwanamke huyo alijitambulisha kwa jina la Henna, na wakati wa tukio alikuwa katika mall ya West gate na wanae wawili pamoja na dereva wakifanya manunuzi ndipo ghafla mashambulizi yakaanza. Wakati wa kujiokoa aliamua kuwa msamaria mwema kwa kumsaidia mwathirika mwenzie aliyejeruhiwa kama ilivyoonekana katika picha iliyozuwa uvumi wa kuwa ‘white widow’.
Mtazame hapa

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MWANAMKE ALIYEFANANISHWA NA KINARA WA MAUAJI YA WESTGATE AJITOKEZA NA KUKANUSHA HABARI HIYO”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.