Thursday, October 3, 2013
EXCLUSIVE: NIYONZIMA AUNGULIWA NA NYUMBA JIJINI DAR, MAJIRANI WAOKOA FAMILIA YAKE
Thursday, October 3, 2013 by Unknown
Kiungo nyota wa Yanga, Haruna Niyonzima ameunguliwa na nyumba yake.
Nyumba anayoishi iko Magomeni jijini Dar es Salaam na moto huo ulianza saa 12 alfajiri hadi ulipozimwa na majirani saa moja asubuhi leo.
Taarifa zinasema nyumba hiyo imeungua kutokana na hitilafu ya umeme katika moja ya nyanya ndani ya nyumba hiyo.
Vitu kadhaa vya thamani ndani ya nyumba yake vimeteketea kwa moto lakini familia yake imesalimika baada ya majirani kuwaokoa.
“Kweli ninawashukuru sana majirani kwa kuonyesha uungwana wa hali ya juu, bila ya wao nyumba yote ingeungua.
“Lakini kuna vitu vichache vimefanikiwa kutoka ila vingi sana vimeungua na moto huo uliokuwa mkali sana,” alisema.
Hadi blogu hii inaondoka eneo la tukio asubuhi hii, baadhi ya watu na mashabiki wa Yanga walikuwa wamefika kwa ajili ya kutoa msaada zaidi.
Pia fundi wa umeme alikuwa anasubiriwa ili kuangalia hitilafu iliyosababisha moto ilitokana na kitu gani.
BY SALEHE JEMBE
Tags:
michezo

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “EXCLUSIVE: NIYONZIMA AUNGULIWA NA NYUMBA JIJINI DAR, MAJIRANI WAOKOA FAMILIA YAKE”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.