Tuesday, March 25, 2014

Hii ndiyo Jumla ya Watanzania waliohukumiwa kunyongwa China.



 
Matukio ya kukamatwa kwa Watanzania nchini China huku wakihusishwa na biashara ya dawa za kulevya yamekua yakitangazwa mara kwa mara huku wengi wao tukipata taarifa za kuwa hukumu yao wamekuwa wakihukumiwa kunyongwa.
 
Katibu Mkuu wa mambo ya Nje John Haule ametaja jumla ya watuhumiwa waliokamatwa kwa kesi ya madawa ya kulevya>>






’Tuna Watanzania wengi tu ambao wapo kwenye magereza kule nchini China tumeshindwa kwa haraka haraka kupata idadi ya waliojihusha na shughuli ya dawa za kulevya’
 
‘Katika Magereza ya China mpaka February tumepewa taarifa na Mamlaka za China kwamba wapo Magerezani Watanzania 177 na katika ya hao 15 wamehukumiwa kunyongwa kutokana na biashara hiyo ya dawa na kukamatwa na dawa hizo lakini niseme tu wenzetu wa Serikali ya China wanatuthamini sana kama sisi tunavyowathamini’
‘Lakini wenzetu wanathamini zaidi mahusiano yetu na ndiyo maana hata wale wachache Watanzania waliohukumiwa kunyongwa kutokana na makosa hayo waliyotenda kule hawajanyongwa mpaka leo na hatutegemei kama watanyongwa sana sana watafungwa kifungo cha maisha’.

Tags:

0 Responses to “Hii ndiyo Jumla ya Watanzania waliohukumiwa kunyongwa China.”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI