Sunday, October 20, 2013

KUWA MAKINI: UTAPELI MWINGINE WAINGIA NCHINI; SASA WANATUMIA MITANDAO YA INTERNET YA KUOMBA AJIRA, TAFADHALI SOMA TAARIFA HII USIJE UKALIZWA


Kuna
UTAPELI mpya umeingia Nchini, kuna watu ambao wanajifanya wana 
makampuni na wanatafuta watu wa kazi namaanisha wanatangaza nafasi za 
kazi, nafasi hizo za kazi huzitangaza kupitia mitandao ya Internet 
ambayo huwa ina maeneo ya kutangaza nafasi za ajira, nitashindwa kuitaja
mitandao hiyo kwa kuwa sio utaratibu ila wewe ambaye unajua kuwa kuna 
mitandao ambayo inatangaza ajira kupitia njia ya Internet ujue ndio hiyo
ambayo tunaiongelea hapa. 

Matukio yenyewe yanakuwaje: Watu hao hutangaza nafasi za kazi 
mbali mbali kupitia mitandao hiyo kwa kuandika wana makampuni na 
wanatafuta watu kwa nafasi mbambali kwenye makampuni yao feki, kwa 
kutambua watanzania wengi wana shida ya ajira hutangaza nafasi ambazo 
wanaamini wengi wataziomba na kuweka vigezo vya chini sana hasa eneo la 
Elimu na uzoefu kwa kuamini wengi wataomba, baada ya hapo, wewe mwenye 
shida ya ajira ukishatuma CV yako ambayo itakuwa pia inaonyesha 
mawasiliano yako, wao hutumia mwanya huo kukutumia ujumbe mfupi (SMS) na
kujifanya wao ni wafanyakazi wa kampuni husika ambayo imetangaza nafasi
hiyo na kujidai wanaweza kukusaidia kuipata kazi hiyo na kukutaka 
uwatumie hela ili wakufanyie mpango na kukutumia maswali ambayo 
utaulizwa kwenye INTERVIEW na majibu yake, hawa jamaa kwa kutambua shida
ya Watanzania hawasemi wanataka kiasi kikubwa huwa wanataka kiasi cha 
Elfu kumi hadi Hamsini, wanafanya hivyo kwa kutambua wewe mtafuta ajira 
unaweza ukakipata kiasi hicho. 
Matapeli hao hudiriki kukwambia na kiasi cha mshahara ambao 
utalipwa kwenye kazi hiyo ili kukutamanisha utume hiyo hela, simu hiyo 
ambayo imekutumia ujumbe huo ukiipigia huwa haipatikani na ikipatikana 
haipokelewi na wanakua wameziregister kwa majina ambayo wanakuaminisha 
ni yao kumbe ni majina ya uongo ya kutapelia watu. 

Mpaka sasa wameshawaliza watu wengi sana kwa hiyo wewe mdau kuwa
makini sana wakati unaomba ajira kupitia mitandao mbalimbali ya 
Internet, ukiona unaombwa hela baada ya kuomba ajira kupitia mitandao 
hiyo ujue ndio hao matapeli. 

KUWA MAKINI EWE MTANZANIA

IMETOLEWA NA:
MDAU MPENDA HAKI
SOURCE;DJSEK

SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO

Tags: ,

0 Responses to “KUWA MAKINI: UTAPELI MWINGINE WAINGIA NCHINI; SASA WANATUMIA MITANDAO YA INTERNET YA KUOMBA AJIRA, TAFADHALI SOMA TAARIFA HII USIJE UKALIZWA”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI