Friday, October 18, 2013
SIMBA "MRISHO NGASSA ANDAA ZIMA MOTO LA KUZIMA NYUMBA ZAKO"
Friday, October 18, 2013 by Unknown
KLABU ya Simba imemtaka kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa, aandae kabisa gari la kuzima moto kwenye nyumba zake kwa kuwa ina uhakika mchezaji huyo hataweza kutimiza ahadi yake ya kufunga au kutoa pasi ya bao.
Simba na Yanga zinakutana keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar na Ngassa ameahidi asipofunga au kutoa pasi itakayozaa bao, basi atazichoma moto nyumba zake tano.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema hawana hofu na Ngassa na kwamba hana hata historia ya kuifunga Simba, hivyo cha msingi aandae zima moto haraka ili kuepuka hasara mapema.
“Siwezi kusema hatatufunga kwa kuwa ni majaaliwa ya kila mtu jinsi Mungu alivyompangia lakini sisi hatuna hofu naye, atambue kuwa hajawahi au hana historia ya kuifunga Simba, ila tunamshauri aandae zima moto mapema, tusijemtia hasara bure,” alisema Kamwaga.
Tags:
michezo

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 Responses to “SIMBA "MRISHO NGASSA ANDAA ZIMA MOTO LA KUZIMA NYUMBA ZAKO"”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.