Monday, December 9, 2013

WASICHANA HAWA WAGUNDUA GENERATOR LINALOTUMIA MKOJO, WACHEKI HAPA










WASICHANA
wanne kutoka Nigeria wamegundua jinsi ambacyo mkojo unaweza kutumika
kama mafuta ya kusukuma jenereta. Wasichana hao, Duro-Aina
Adebola,Akindele Abiola, Faleke Oluwatoyin na Bello Eniola, wote wenye
umri wa miaka 14 wamefanya maonyesho ya jenereta hilo na limeonekana kufanya kazi.

Genereta
hilo linaweza kufanya kazi kwa muda wa saa moja likitumia lita moja tu
ya mkojo. Linauwezo wa kuendesha vifaa vinavyotumia umeme wa kati kama
vile taa, jokofu, redio, televisheni n.k, Sasa genereta hilo linafanyaje
kazi?

Kwanza mkojo huo unawekwa kwenye chombo kiitwacho
electolytic cell, ambacho hutenganisha mkojo huo na hydrogen. Kisha
hydrogen hiyo huenda moja kwa moja kwenye chujio la maji kwaajili ya
kuisafisha na kisha kuisukuma katika gas cylinder.

Hiyo gas
cylinder nayo huisukuma hydrogen mpaka katika kitu kinachoitwa, liquid
borax ambayo huisukuma hewa hiyo na kuliwezesha jenereta kufanya kazi.

SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO

Tags:

0 Responses to “WASICHANA HAWA WAGUNDUA GENERATOR LINALOTUMIA MKOJO, WACHEKI HAPA”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI