Saturday, March 29, 2014
SHIRIKISHO LA FILAMU TANZANIA "HATUITAMBUI BONGO MOVIE UNITY YA STEVE NYERERE"
Saturday, March 29, 2014 by Unknown
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania(TAFF) Simon Mwakifwamba amedai shirikisho lake haliwatambui wasanii wanaounda kundi la Bongo Movie Unity na kudai kuwa kundi hilo linaundwa na watu sita tu huku wengine wakifuata mkumbo.
Akizungumza na Global Publishers, Mwakifwamba ambaye pia ni muigizaji wa muda mrefu na muongozaji wa filamu amesema hawatambui wasanii hao na anawashauri wajiunge ili watambulike. “Bifu la nini? Mimi ni baba, wao ni watoto. Kwanza sikia… wale sio wanachama wangu.Nawashauri wajiunge kwenye vyama vyangu ili niwatambue kama sehemu ya shirikisho,” alisema.
“Kwanza Bongo Muvi si chama kama wengi wanavyofikiri, ni kampuni na ina wamiliki wake tisa, hao wengine wanafuata mkumbo kwa sababu hawajitambui. Kama wanabisha, waonyeshe usajili wao wa Basata, maana chombo pekee kinachosajili kazi za wasanii ni Basata.”
Hata hivyo Bongo5 imejaribu kumtafuta mwenyekiti wa BMU, Steve Nyerere kuzungumzia kauli hiyo, lakini amekuwa hapokei simu.
-Bongo5 Tags: celebrities

This post was written by: Author Name
Author description goes here. Author description goes here. Follow him on Twitter
Get Updates
Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.
Related Articles
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SHIRIKISHO LA FILAMU TANZANIA "HATUITAMBUI BONGO MOVIE UNITY YA STEVE NYERERE"”
Post a Comment
Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.