Wednesday, March 26, 2014

MLINZI WA OBAMA AFANYA KUFURU NA VIHOKA JUU....


 
Jarida la Washington Post nchini Marekani limeripoti kwamba askari watatu ambao ni walinzi wa president wameachishwa kazi kwa muda na kurudishwa nyumbani ili uchunguzi ufanyike.
Askari mmoja kati ya hao alikutwa amelewa pombe chakari kwenye hoteli moja huko Amsterdam ambapo Obama alienda kwa ajili ya mkutano wa mambo ya Nuclear.
Msemaji wa idara ya upelelezi Marekani alikataa kutoa taarifa zaidi kuhusu tukio hilo ingawa alisisitiza kuwa watatu hao wameachishwa kazi kwa muda huku uchunguzi ukiendelea.
Mwaka 2013 majasusi wawili waliondolewa katika kikosi cha ulinzi cha Rais Obama kufuatia tuhuma za kuhusika na kashfa ya ngono na utovu wa nidhamu.
Mwaka 2012 majasusi kadhaa waliachishwa kazi kufuatia madai kuwa walikodi makahaba walipokuwa mjini Cartagena Colombia.

Tags:

0 Responses to “MLINZI WA OBAMA AFANYA KUFURU NA VIHOKA JUU....”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI