Thursday, December 5, 2013

HUZUNI: Raisi wa Zamani wa Afrika Kusini ndugu NELSON MANDELA AMEFARIKI DUNIA jana baada ya kuugua kwa muda mrefu.







Raisi wa zamamni wa Afrika ya kusini bwana Nelson Mandela amefariki dunia jana jioni akiwa na miaka 95 baada ya kuugua na luzwa kwa muda mrefu hospitalini alipokuwa akipatiwa matibabu.


Taarifa rasmi toka serikali ya Afrika kusini zimethibitisha kifo hicho cha ndugu Mandela na tayari raisi wa Afrika kusini mr. Jacob Zuma ametuma salamu za rambirambi kwa familia na wanachi wote wa afrika ya kusini na duniani kwa ujumla walioguswa na kifo hiki.


Mandela atakumbukwa kama mfano na alama ya Afrika kwa kuongoza mapambano makubwa dhidi ya ubaguzi wa Rangi nchini Afrika kusini na Afrika kwa ujumla.


Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amen

Tags: ,

0 Responses to “HUZUNI: Raisi wa Zamani wa Afrika Kusini ndugu NELSON MANDELA AMEFARIKI DUNIA jana baada ya kuugua kwa muda mrefu.”

Post a Comment

Ila tafadhali sana angalia usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu.

HHHHHHHHHHHH

Subscribe

Kwa habari na Taarifa weka Email yako Hapa tutakutumia

© 2014 FUNUNU HABARI.. All rights reserved.
Designed by FUNUNU HABARI